Tuesday 5 August 2014

AJALI YA BASI BUNDA

 Toyota Coaster lenye namba za usajili T 399 BYC lililokuwa likitokea Musoma kwenda Bunda likiwa limepata ajali mchana huu eneo la Bitaraguru, Bunda mkoani Mara.
Baadhi ya abiria walionusurika katika ajali wakisaidiwa kutoka kwenye basi hilo.
Wananchi wakishuhudia ajali hiyo.
Basi hilo likiinuliwa na wananchi baada ya ajali.
BASI la abiria aina ya Toyota Coaster lenye namba za usajili T 399 BYC lililokuwa likitokea Musoma kwenda Bunda limepata ajali mchana huu na kujeruhi abiria katika eneo la Bitaraguru lililopo nje kidogo ya mji wa Bunda mkoani Mara.