Saturday, 22 March 2014

MOURINHO ASHITAKIWA ENGLAND!!!!!

                                            
  
 Kufuatia kipigo walichokipata wiki iliyopita kutoka kwa Aston Villa cha bao 1-0, Kocha mkuu wa klabu ya chelsea merno Jose Mourinho amejikuta yuko hatiani baada ya kile kinachodaiwa ni utovu wa nidhamu.

Katika pambano hilo Mourinho alijikuta anatolewa nje ya uwanja,kwa kitendo chake cha  kuingia ndani ya uwanja kuongea na mwamuzi Chris Foy baada ya kiungo wake wa kibrazil Ramires kuonyeshwa kadi nyekundu dakika za lala za salama.
Mourinho ameamriwa mpaka Jumatatu awe amejibu tuhuma kwa Chama cha Soka England.Mreno huyo, ambaye pointi za uongozi katika ligi zilipunguzwa kufuatia kipigo hicho, alimlaumu mwamuzi Foy baada ya mchezo katika uwanja wa Villa Park.