Friday 24 April 2015

Hii ndio list ya Marais 8 wa Afrika wanaoongoza kwa utajiri

plane-red-carpetKuna tafiti mbalimbali zilizowahi kufanywa, lakini leo nimekuja na hii list ya Marais nane wanaoongoza kwa kuwa na utajiri mkubwa zaidi ya wenzao Afrika.
Iko ishu ya Marais kung’ang’ania madaraka kwenye nchi za Afrika, kingine ni hii ishu ya kujilimbikizia mali, japo wapo wanaokuwa nazo kabla ya kushika madaraka lakini wengine wanajichumia hapohapo wakiwa madarakani.
dos
Jose Eduardo Dos Santos ndiye Rais anayeongoza kwa utajiri Afrika. Ni Rais wa Angola, aliingia madarakani mwaka 1979,  utajiri wake ni dola bilioni 20
MOROCCO-SARKOZY-MOHAMED-VI
Mohammed VI- Ni Mfalme wa Morocco ambaye amekaa madarakani
kwa miaka 15, ana utajiri wa dola bilioni 2.
ekwa
Teodoro Obiang Nguema Mbasogo: Huyu ni Rais wa Equatorial Guinea, aliingia madarakani 1979.. ana una utajiri wa dola milioni 600. Nchi yake ni moja ya nchi ambazo ni maskini sana lakini huo ndio utajiri wake mwenyewe.
kenya
Uhuru Kenyatta ni Rais wa Kenya. Kaingia madarakani mwaka 2011, utajiri wake ni dola milioni 500. Mbali ya kuwa Rais ana miradi mingi pamoja na hisa kwenye Mabenki makubwa na mahoteli ya kifahari.
biya
Paul Biya ni Rais wa Cameroon tangu mwaka 1982, ana utajiri wa dola milioni 200, unaambiwa ndiye rais anayetumia kiasi kikubwa cha pesa katika ziara zake kuliko marais wote duniani. Ziara yake kwa siku moja ni kama Euro 30,000 hivi.
king
King Mswat iii Ni mfalwe wa Swazland akiwa na utajiri wa dola milioni 100, anashika nafasi ya 15 katika familia za kifalme tajiri duniani, Unaambiwa wake zake 13 hutumia zaidi ya dola milioni sita kufanya manunuzi yao pekee, pia Serikali yake hutenga bajeti ya dola milioni 61 kila mwaka kwa ajili ya matumizi ya nyumbani
dd
Idriss Derby Ni Raisi wa Chad tangu mwaka 1990 na ana utajiri wa zaidi ya dola milioni 50
mugabe
Robert Mugabe wa Zimbabwe, ana zaidi ya miaka 26 akitawala nchi hiyo. Utajiri wake ni dola milioni 10