Friday, 4 April 2014

Breaking nwzz: Watatu wafariki kwa kufukiwa kifusi machimboni Dar

Shughuli ya uokoaji ikiendelea.

Waokoaji baada ya kugundua mwili ulipo.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo.
Watu waliofika eneo la tukio kuwatambua marehemu.
Mwili baada ya kufukuliwa.
Wasamaria wema wakienda kuuhifadhi mwili.
Watu watatu waliofahamika kwa majina ya Msagala, Jacob na Mhando wakazi wa Bunju jijini Dar es Salaam mchana huu wamefariki dunia.
Baadhi ya kinamama wakiwa na nyuso za huzuni.
Gari la kampuni ya mmiliki machimbo.
WATU watatu waliofahamika kwa majina ya Msagala, Jacob na Mhando wakazi wa Bunju jijini Dar es Salaam mchana huu wamefariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba kokoto kwenye machimbo ya Mtanzania mwenye asili ya Kiasia aliyefahamika kwa jina la Kara Arjan yaliyopo Bunju-Mbweni jijini.
Habari zilizopatikana eneo la tukio zilisema kuwa machimbo hayo yalishapigwa marufuku kutokana na watendaji wake kufanya kazi katika mazingira hatarishi. Wachimbaji hao wakiwa kazini, sehemu ya machimbo hayo iliporomoka na kuwafukia.