Monday, 24 March 2014

Alichosema Cristiano Ronaldo baada ya kufungwa na Barca hiki hapa


382168_heroa
Cristiano Ronaldo amezungumza baada ya kipigo cha jana kutoka FC Barcelona akisema walikuwa wakicheza Barca yenye wachezaji 12.

Mwanasoka huyo bora wa dunia amesema kwamba refa wa mchezo huo Undiano Mallenco alichangia timu yake kupoteza wa El Clasico hapo jana usiku katika dimba la Santiago Bernabeu.
Madrid walipewa penati ya utata muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza, lakini Mallenco aliwapa Barca penati mbili muda mfupi baadae — pia alimtoa kwa kadi nyekundu Sergio Ramos – na Ronaldo anasema anahisi refa alikuwa akiwapendelea Barcelona kwa makusudi.