Friday, 7 February 2014

TUNAOMBA RADHI KWA PICHA::MTU MMOJA AKUTWA AMEJINYONGA UFUKWE WA SPICE HOTEL

Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Bahati maarufu kwa uuzaji wa mifuko ya plastiki maeneo ya stand kuu ya mabasi Bukoba amekutwa kajinyonga juu ya mti  maeneo ya ufukwe wa Spice Motel majira ya saa nane mchana ..
Taarifa za awali  kutoka kwa watu waliokuwa katika tukio hilo zinasema  kuwa , kabla ya kifo cha, marehemu alionekana akiwa na mafurushi ya vitu na alikuwa akifua katika eneo hilo la ufukwe...
Mtu mmoja ambae hakuwa tayari kutaja jina lake  ameueleza  mtandao  huu  kuwa  leo majira ya saa 12.00asubuhi alisalimiana na marehemu maeneo ya stand ya mabasi akiendelea na shughuli yake ya kutembeza mifuko ya plastiki kwenye mabasi yaendayo  mikoani na maeneo mengine akiwa mzima wa afya.
Mwili wa marehemu umepelekwa Hospital ya Mkoa  wa Kagera kuifadhiwa kwa ajili ya utambuzi ( ndugu zake )
 Askari akiwa amepanda mti ili aweze kukata kamba aliyotumia kujinyonga
 
 Amekutwa katika hali hii
 
 
 Haijafahamika ni kwa nini kachukua maamuzi haya
 
 
 
 
 Mwili wa marehemu ukishushwa
 
 
 Kamanda wa polisi wilaya ya Bukoba akishuhudia tukio
 
 
 Wananchi waliokusanyika katika tukio
 
 
 
 
 
 
 Mkuu wa kituo cha polisi Bukoba(mwenye koti) akiwa anaangalia baadhi uya vitu vya marehemu alivyokuja navyo kabla ya kujinyonga
 
 
 Hivi ni vitu vya marehemu alivyokuja navyo babla ya kujinyonga
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 Maeneo ya spice beach
 
 
 Mmoja wa watu wa kwanza kutoa taarifa kituo cha polisi Mama Faima
 
 
 
 
 Mwili wa marehemu ukipakiwa kwenye gari la polisi
 
 
Mwili wa marehemu ukipelekwa kuifadhiwa hospital ya mkoa wa kagera