Katika taarifa iliyotolewa jana Jumapili, polisi wa Cairo walisema kwamba itapambana na jaribio lolote la mashabiki kujaribu kuingia uwanjani.
Azmi Megahed, msemaji wa FA ya Misri, alisema raia hawatoruhusiwa kuhudhuria mechi hiyo kutoka sababu za kiusalama.
Jumamosi wiki iliyopita, polisi walipambana na mashabiki wa Zamalek White Knights ambao walijaribu kuingia katika uwanja wa Cairo kuangalia mchezo kati ya Zamalek dhidi ya mabingwa wa Angola Cabo Schrob. Fujo hizo zilipelekea kwa kukamatwa kwa mashabiki 33.