Friday, 28 February 2014

AJALI MBAYA YA GARI YAMKUTA MCHUNGAJI MICHAEL, JIONEE MWENYEWE



Mch Michael Zacharia Twakaniki (katikati)akiwa hospitalini huko Dodoma kushoto mwenye tai ni Mhazini wa jimbo la Mashariki mwa Tanzania katika kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzania Athanas Sigoma alipomtembelea jana 

Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Dodoma Michael Zachariah Twakaniki alipata ajali Februari 25,2014 ya gari ambalo alikuwa akiliendesha akiwa na abiria wenzake 6,wawili wakiwa ni watoto wake,wajukuu wawili na rafiki zao wawili.
Ajali hiyo ilitokea eneo la Chamwino Dodoma,walipokuwa wakisafiri kuelekea Dodoma toka jijini Dar es salaam.
Ajali hiyo inaelezwa ilitokea baada ya kumkwepa mwendesha baiskeli na gari hilo kubiringita mara nne.
 
CHANZO: MTANGAZAJI MADUHU BLOG