Thursday, 27 February 2014

KIKONGWE WA MIAKA 70 AFA KWA KUGONGWA NA GARI IRINGA

Mwili wa mtoto aliyegongwa na gari hivi karibuni mjini  Iringa (picha na maktaba ya matukiodaima.com
Mwandishi  Diana Bisangao wa matukiodaima.com Iringa 
Mtu mmoja jina bado halijafahamika mwenye umri kati ya miaka 60 hadi 70 amefariki dunia baada ya kugongwa na gari maeneo ya barabara kuu ya Iringa - Mbeya.
Akizungumza ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhani Mungi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 26 februari majira ya saa 3:45 usiku.
Kamanda Mungi aliitaja gari iliyomgonga marehemu ni aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajili T.731 AAU iliyokuwa ikiendeshwa na dereva asiyejulikana huku chanzo kikiwa ni mwendo kasi. Dereva anatafutwa.